Tangazo la Nafasi za Ajira
Hospitali ya Wasso - Jimbo Kuu Katoliki Arusha
Wilaya ya Ngorongoro
a). SIFA ZA MWOMBAJI
- Awe na cheti cha kidato cha nne au kidato cha sita, Astashahada ((EN) Enrolled Nurse) na Stashahada ((ANO) Assistant Nursing Officer) ya Nursing and
- Midwifery kutoka chuo kinachotambulika na NACTE
- Awe amesajiliwa na Baraza la Uuguzi na Ukunga Tanzania (TNMC)
- Awe na leseni hai ya kufanya kazi (Valid Practicing license)
- Uzoefu wa kazi ya uuguzi katika mazingira ya vijijini utapewa kipaumbele
- Maadili mema, uwezo wa kufanya kazi kwa timu na kuhudumia kwa huruma.
b). MAJUKUMU YA KAZI
- Kutoa huduma za uuguzi kwa wagonjwa wa aina mbalimbali kwa kufuata miongozo ya kitabibu
- Kutoa huduma za Afya ya uzazi kwa wanawake wajawazito kabla na baada ya kujifungua.
- Kusimamia na kusaidia mama wakati wa leba na kujifungua kwa kuzingatia taratibu salama za kitabibu.
- Kufuatilia maendeleo ya Afya ya mama na mtoto mchanga baada ya kujifungua, na kutoa ushauri wa kitaalamu.
- Kutoa elimu ya Afya kwa wanawake kuhusu lishe , uzazi wa mpango ,kunyonyesha , usafi wa mwili na mazingira.
Deadline: 28th February 2026
Hospitali ya Wasso - Jimbo Kuu Katoliki Arusha
Wilaya ya Ngorongoro
a). SIFA ZA MWOMBAJI
- Awe na cheti cha kidato cha nne au kidato cha sita, Diploma ya Radiology/Medical Imaging kutoka chuo kinachotambulika
- Awe amesajiliwa na Baraza la wataalamu wa mionzi Tanzania
- Awe na leseni halali ya kazi
- Awe na Ujuzi wa kutumia mashine za digital X-ray, Utrasound
- Awe na Uwezo wa kufanya kazi kwa kujitegemea na kwa kufuata maadili ya kazi.
b). MAJUKUMU YA KAZI
- Kuchukua picha za ndani ya mwili wa binadamu kwa kutumia mionzi (kama X-ray).
- Kumwandaa na kumuelekeza mgonjwa kabla na wakati wa upigaji wa picha
- Kuhakikisha usalama wa mgonjwa dhidi ya madhara ya mionzi kwa kutumia vifaa vya kujikinga na kudhibiti kiasi cha mionzi
- kinachotumika Kuendesha na kudhibiti vifaa vya mionzi ili kuhakikisha vinafanya kazi kwa usahihi.
- Kuhifadhi na kuwasilisha picha na taarifa za uchunguzi kwa wataalamu husika.
- Kudumisha usiri na heshima kwa wagonjwa.
Deadline: 28th February 2026
Hospitali ya Wasso - Jimbo Kuu Katoliki Arusha
Wilaya ya Ngorongoro
DAKTARI DARAJA LA II (MEDICAL DOCTOR II) NAFASI (1)
a) SIFA ZA MWOMBAJI
- Awe amehitimu Shahada ya Udaktari (MEDICAL DOCTOR)
- Awe amesajiliwa na Baraza la Madaktari Tanganyika (Medical Council of Tanganyika - MCT).
- Awe na leseni halali ya kufanya kazi.
- Awe na uzoefu wa kazi (uzoefu utazingatiwa )
- Awe na maadili mema, bidii, na uwezo wa kufanya kazi kwa kushirikiana na wengine
b) MAJUKUMU YA KAZI
- Kutoa huduma za uchunguzi na matibabu sahihi kwa wagonjwa.
- Kusimamia na kufuatilia maendeleo ya wagonjwa.
- Kushirikiana na timu ya wahudumu wa afya kuboresha huduma.
- Kutunza kumbukumbu sahihi za wagonjwa.
MASHARITI YA JUMLA
- Mwombaji awe ni Raia wa Tanzania na mwenye umri usiozidi miaka 45.
- Cheti cha mtihani wa kidato cha IV na VI.
- Mwombaji aambatishe nakala ya cheti cha kuzaliwa, Kitambulisho cha Taifa (NIDA) au kitambulisho cha mpiga kura.
- Mwombaji aambatishe maelezo binafsi yanayojitosheleza yenye anwani na namba za simu za kuaminika pamoja na majina ya wadhamini (Referees) watatu wa kuaminika.
- Mwombaji aambatishe maelezo binafsi yanayojitosheleza yenye anwani na namba za simu za kuaminika pamoja na majina ya wadhamini (Referees) watatu wa kuaminika.
Deadline: 28th February 2026
Hospitali ya Wasso - Jimbo Kuu Katoliki Arusha
Wilaya ya Ngorongoro
HOSPITALI YA WASSO - JIMBO KUU KATOLIKI ARUSHA
WILAYA YA NGORONGORO
Hospitali ya Wasso ni hospitali ya kanisa jimbo kuu katoliki la Arusha inayotoa huduma za afya kwa jamii ya Ngorongoro na maeneo ya jirani.
Mganga Mfawidhi Hospitali ya Wasso anakaribisha maombi ya kazi kwa kada ya Afisa Hesabu Daraja la II.
1. AFISA HESABU DARAJA LA II (ACCOUNTS OFFICER II) NAFASI (1)
a) SIFA ZA MWOMBAJI
• Awe na Shahada ya Uhasibu, Fedha, Uchumi au fani inayohusiana kutoka chuo kinachotambuliwa na Serikali
• Awe mwenye CPA (T) au sifa nyingine inayolingana na kutambuliwa na Bodi ya Wahasibu na Wakaguzi (NBAA).
• Awe amesajiliwa na NBAA kama Certified public Accountant.
• Awe na ufahamu wa mifumo ya kifedha ya Serikali na Mifumo mingine ya Kiteknolojia ya uhasibu
• Awe na uwezo mzuri wa kutumia kompyuta, hasa programu za uhasibu na MS Office (Word, Excel, Outlook).
• Awe na uzoefu au uelewa wa masuala ya fedha katika Sekta ya Afya.
• Awe na uwezo wa kufanya kazi kwa umakini, uadilifu, uaminifu na kwa kufuata taratibu za kifedha.
• Awe na mawasiliano mazuri, nidhamu, na uwezo wa kufanya kazi kwa kushirikiana na wengine.
b) MAJUKUMU YA KAZI
• Kuandaa na kutunza kumbukumbu za fedha za Hospitali kwa mujibu wa kanuni na taratibu.
• Kuhakikisha Mapato na Matumizi yote ya fedha yanarekodiwa ipasavyo kwenye mifumo ya uhasibu.
• Kuandaa hatimiliki. Vocha, Risiti, Malipo na nyaraka zote za kifedha.
• Kufanya upatanisho wa akaunti (Bank Reconciliation) kila mwezi.
• Kushiriki katika kuandaa bajeti ya mwaka, tathmim ya bajeti na taarifa za fedha za robo mwaka na mwaka mzima.
• Kuandaa na kuwasilisha taarifa za kifedha kwa uongozi wa Hospitali.
• Kufanya uhakiki'wa madai kabla ya kufanyika kwa malipo.
• Kushiriki katika ukusanyaji na ufuatiliaji wa mapato ya Hospitali
Deadline: 31st December 2025
Hospitali ya Wasso - Jimbo Kuu Katoliki Arusha
Wilaya ya Ngorongoro
Deadline: 30th November 2025
Hospitali ya Wasso - Jimbo Kuu Katoliki Arusha
Wilaya ya Ngorongoro
MPISHI DARAJA LA II (COOK GRADE II) NAFASI (1)
a) SIFA ZA MWOMBAJI
- Awe na cheti cha kidato cha nne au kidato cha sita.
- Awe na Cheti cha Hotel Management kutoka chuo kinachotambulika na Serikali.
- Awe na uzoefu wa angalau miaka miwili (2) katika Hoteli, Lodge au hosteli ya kitalii.
- Uwezo wa kuandaa vyakula vya kimataifa (Continental & African dishes) utapewa kipaumbele.
- Awe na uelewa wa masuala ya usafi wa chakula, huduma kwa wateja (Customer care), na usalama wa chakula (Food safety standards).
- Awe na maadili mazuri, Mwaminifu, mchapakazi, na mwenye uwezo wa kufanya kazi kwa muda mrefu kulingana na ratiba ya wageni
b) MAJUKUMU YA KAZI
- Kupika na kuandaa chakula bora kwa wageni na watalii wanaofikia katika Hospitali yetu kwa kuzingatia viwango vyenye ubora.
- Kuandaa menyu mbalimbali (Local & continental dishes) kulingana na mahitaji ya wageni.
- Kuhakikisha sehemu ya jikoni, vyombo na vifaa vya upishi vinakuwa safi muda wote. • Kusimamia upokeaji, uhifadhi na matumizi sahihi ya malighafi za chakula.
- Kuhakikisha huduma za chakula zinatolewa kwa wakati, kwa usafi na kwa ukarimu.
- Kushirikiana na Uongozi katika kuboresha huduma na kuridhisha wateja.
- Kuhakikisha gharama za upishi zinadhibitiwa na kuzingatia bajeti ya mapato ya hostel.
Deadline: 28th February 2026
